
Mwanafunzi aliyekuwa akisoma  
shule  ya  sekondari  Sabasaba  mjini  Iringa akijiandaa kurudia  
kufanya  mtihani  wa  taifa  wa kidato  cha nne kupitia  kituo  cha 
Krelluu mjini  Iringa Khamis Mkundo  mkazi  wa Mwangata  C katika 
manispaa ya  Iringa amejiua kwa kujinyonga  kwa kamba kwa kile  
alichodai  kuchoshwa na kufeli  mara kwa mara mtihani wa kidato cha nne.
Katika  barua  yake  ndefu 
aliyoiandika  kijana  huyo amesema  kuwa amefanya  hivyo si kwa 
kujipendea  ila amechukizwa na hatua yake ya  kufeli mara kwa mara  
hivyo  kuamua  kujiua ili  kuepuka aibu katika mtihani ujao ambao 
anaamini angefeli.
Shemeji  wa  kijana  huyo Aden Tagalile 
ameueleza mtandao  matukiodaima.com  kuwa  tukio  hilo 
limetokea mida ya saa 12 na saa 1  usiku wa  leo baada ya 
kuwepo kwa mazungumzo ya muda  mrefu  kwa kijana  huyo kuonyesha 
kuchukia hatua yake ya kuendelea kuristi  mtihani  wa kidato cha nne  
bila mafanikio.
Kijana huyo  alisema hajapenda  kuona anaendelea  kufeli na kuwa  yupo tayari kwa lolote  kukwepa aibu ambayo ipo mbele  yake.
Hata  hivyo kufuatia mazungumzo hayo, kijana huyo aliagana na ndugu zake akiwemo kaka  yake anayeishi nae kwa
 kila mmoja kuondoka nyumbani  hapo kabla  ya kijana  huyo kukutwa 
amejinyonga.
Mwenyekiti  wa serikali  ya mtaa huo 
Sarehe Mgimwa amethibitisha  kutokea kwa kifo  hicho na kuonyesha ujumbe
 ambao kijana  huyo ameuacha .
-Matukiodaima .com







