Like Us On Facebook

MUME AMSHITAKI MKEWE KWA KUMZALIA WATOTO WENYE SURA MBAYA ASHINDA KESI NA KULIPWA TSH.192,840,000



Mwanaume wa China ameshinda kesi ya kulipwa $120 000 ( tsh.192, 840,000/=) baada ya kumpa taraka mke wake kwa kumzalia watoto wabaya.
 
Awali, mwanaume huyo aitwaye Jian Feng, alikuwa akimtuhumu mke wake kuwa anatoka nje ya ndoa kwakuwa haikuwa ikimuingia akilini kuzaa watoto wasiovutia kama wao..
 
Baada ya DNA kuweka bayana kuwa kweli watoto ni wa kwake, mke wa Feng aliamua kuitoa siri nyingine ndogo.

Kabla ya wanandoa hao kukutana, mke wa Feng alikuwa amefanyiwa upasuaji wa urembo (cosmetic surgery) uliogharimu $100,000 nchini Korea Kusini na ndio maana watoto waliozaliwa walikuwa tofauti na wazazi.
 
Feng alimshitaki mke wake kwa kuficha ukweli huo na kumfanya amuone mrembo. Kutokana na maelezo hayo, jaji alimpa ushindi Feng na kumwamuru mke wake amlipe fidia ya dola $120,000.
 
Akiongea na Irish Times, Feng alisema: “Nilimuoa mke wangu kwa upendo, lakini mara baada ya kupata mtoto wa kwanza tulianza kuwa na migogoro. Binti yetu alikuwa mbaya haswaa, hadi kufikia wakati akawa ananitisha.”
TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari