Like Us On Facebook

MAMA KANUMBA ATOA ONYO KALI KWA WANAOTUMIA JINA LA MWANAE KUJINUFAISHA

               MAMA wa marehemu Steven Kanumba, Flora Mtegoa ametoa onyo kali kwa watu wanaotumia jina la mwanaye huyo kuuza filamu zao.
Akichonga na paparazi wetu, Mama Kanumba alisema hivi karibuni kuna filamu imetoka kwa watoto wa baba Kanumba waliopo Shinyanga ambayo imewekwa nembo ya kampuni ya mwanaye, Kanumba The Great Film hivyo haitambui.
“Jamani kampuni ya Kanumba haina tawi Shinyanga kama filamu hiyo inayosambazwa huko bali hiyo imechezwa na watu ambao hawatambuliki katika kampuni ya marehemu mwanangu,” alisema Mama Kanumba.

-GPL
TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari