Like Us On Facebook

WAREMBO MBARONI KWA KULEWA POMBE ZA KIENYEJI MUDA WA KAZI

Washitakiwa wakipelekwa kizimbani.
Afande akimlinda mmoja wa washitakiwa.
Wakisubiri kusomewa mashitaka.
WAREMBO wanne jana wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Sokoine Drive (Jiji) jijini Dar es Salaam kwa kosa la kunywa pombe za kienyeji muda wa kazi.
Warembo hao walinaswa maeneo ya Pugu nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam. Baada ya kufikishwa mahakamani hapo na kukana mashitaka hakimu aliyekuwa akisikiliza kesi hiyo, Timothy Lyon, aliwawekea wazi dhamana kwa kumtaka kila mmoja kuwa na wadhamini wawili na dhamana ya shilingi laki mbili kila mmoja. Sharti hilo la dhamana lilikuwa gumu kwa warembo hao ambao walipandishwa karandinga na kupelekwa Gereza la Segerea mpaka tarehe 15 mwezi ujao.
-GPL
TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari