
Mmoja wa wateja hao ambaye hii ni siku pili kushinda na kulala hapo akisubiri kujipatia simu yake mara zitakapoanza kuuzwa, amesema mpaka sasa ameshakataa ofa ya £200 (515,000 Tsh) kwaajili ya kuuza nafasi yake kwenye foleni hiyo na kuwa na matarajio ofa inaweza kuja kufikia £1000(2,575,000)baadaye.


Vijana hao wawili ambao wameweka kambi jana usiku nje ya duka la Apple wamedai kuwa siku zote wao huwa miongoni mwa wateja wa kwanza kuzipata simu mpya za iPhone kila zinapotoka, hivyo wameamua kuweka kambi nje ya duka ili wahakikishe wawe wateja wa kwanza kuzinunua siku ya Ijumaa.
-BONGO5