Like Us On Facebook

WADAU WA IPHONE 5S WAWEKA KAMBI NJE YA DUKA LA APPLE SIKU 4 KABLA HAZIJAANZA KUUZWA

                 ‘Die Hard customers’ wa simu za iPhone wameamua kupanga foleni nje ya duka la simu hizo jijini London, Uingereza na kuamua kuweka kambi ya muda kwa kufunga matenti na kuhamishia makazi yao hapo huku wakisubiri siku rasmi ya kuanzwa kuuzwa kwa toleo jipya la iPhone5S linalosubiriwa kwa hamu kote ulimwenguni ambayo ni Ijumaa hii (September 20).
iphone 5SIphone 5S zitakazokuwa zikipatikana katika rangi tatu
Mmoja wa wateja hao ambaye hii ni siku pili kushinda na kulala hapo akisubiri kujipatia simu yake mara zitakapoanza kuuzwa, amesema mpaka sasa ameshakataa ofa ya £200 (515,000 Tsh) kwaajili ya kuuza nafasi yake kwenye foleni hiyo na kuwa na matarajio ofa inaweza kuja kufikia £1000(2,575,000)baadaye.
iphone fan-2
iPhone fan-3
Vijana hao wawili ambao wameweka kambi jana usiku nje ya duka la Apple wamedai kuwa siku zote wao huwa miongoni mwa wateja wa kwanza kuzipata simu mpya za iPhone kila zinapotoka, hivyo wameamua kuweka kambi nje ya duka ili wahakikishe wawe wateja wa kwanza kuzinunua siku ya Ijumaa.
-BONGO5
TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari