Like Us On Facebook

WAAMUA KUTUMIA KONDOMU KUJIKINGA NA UGONJWA WA BARIDI

             Watu wa umri wa makamo nchini Afrika Kusini wamebuni mbinu mpya ya kutumia mafuta ya kwenye mipira ya kiume (condoms/kondomu) kwa ajili ya kujitibu maradhi ya baridi yabisi ambayo yamekuwa yakiwasumbua wengi na wamekuwa wakipanga kwenye maungio ya viungo.

Wagonjwa wengi wanaokabiliwa na maradhi ya baridi yabisi wameacha kutumia vidonge ambavyo wamekuwa wakipewa mahospitalini na badala yake wameanza kutumia mafuta hayo kupanga sehemu za maungio ya mwili kwa kuwa

wanapata ahueni ya haraka.

Watu wengi wa umri wa makamo wamekuwa vinara wa kuchukua kondomu ambazo zinasambazwa bure nchini Afrika Kusini kutokana na nchi hiyo kuwa na maambukizi makubwa ya magonjwa ya ngono na virusi vya UKIMWI lakini matumizi yake yamekuwa si ya kuzuia kusambaa kwa ugonjwa huo tena.

Utafiti uliofanyika huko Soweto umethibitsha watu wengi wa makamo wanatumia zaidi mafuta hayo katika kupambana na maumivu yanayochangiwa na baridi yabisi ambayo imekuwa ikiwasumbua mno watu wenye umri mkubwa.

Wazee wengi wamesema kutokana na kupatikana kwa urahisi kwa kondomu kwao imekuwa ni kitu cha faraja kwa sababu wameweza kupata tiba mbadala ya kupaka kwenye maungio mwilini badala ya kuendelea kunywa dawa kila siku.
TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari