Muargentina huyo pamoja na kufunga mabao matatu peke yake usiku, pia alitengeneza bao la nne lililofungwa na Gerard Pique.
Haikuwa bahati yao, Ajax kwani walikosa hadi penalti baada ya kipa Victor Valdes kuokoa mkwaju wa Kolbeinn Sigthorsson.Messi alifunga mabao yake katika dakika za 22, 55 na 75, wakati Pique alifunga dakika ya 69.Kikosi cha Barcelona kilikuwa: Valdes, Alves, Pique/Bartra dk80, Mascherano, Adriano, Busquets, Fabregas/Xavi dk72, Iniesta, Sanchez, Messi, Neymar /Pedro dk72.Ajax: Vermeer, van Rhijn, Denswil, Moisander/van der Hoorn dk73, Blind/Schone dk78, Poulsen, de Jong/Serero dk59, Duarte, Bojan, Sigthorsson na Boilesen.

Mkwaju: Messi alifunga bao la kwanza kwa shuti la mbali la mpira wa adhabu

La pili: Messi akifunga bao lake la pili

Kiulaini: Messi akimtoka beki Stefano Denswil

Tabasamu: Messi akishangilia na beki wake, Dani Alves

Sergio Busquets akidhibiti mpira katikati ya wachezaji wa Ajax, Siem de Jong (kushoto) na Lerin Duarte

Anakosa: Kolbeinn Sigthorsson alikosa penalti iliyochezwa na kipa Victor Valdes

Alexis Sanchez akimvaa Daley Blind wa Ajax Uwanja wa the Camp Nou

Beki wa Barcelona, Adriano akimdhibiti Ricardo van Rhijn wa Ajax

Pique akienda hewani kuifungia Barcelona bao la tatu

Hasira: Neymar aking'aka baada ya kupoteza nafasi ya kufunga

Marafiki wa zamani: Javier Mascherano akichuana na Bojan Krkic anayecheza kwa mkopo

Wako vizuri: Barca wakishangilia ushindi wao Camp Nou
Katika mchezo mwingine wa kundi hilo, AC Milan iliichapa Celtic 2-0 Uwanja wa San Siro, mabao ya Zapata dakika ya 82 na Muntari dakika ya 85.
Kikosi cha AC Milan kilikuwa: Abbiati, Zaccardo, Zapata, Mexes, Constant/Robinho dk76, Nocerino, De Jong, Muntari, Birsa/Emanuelson dk64, Matri/Poli dk87 na Balotelli.
Celtic: Forster, Lustig, Van Dijk, Ambrose, Izaguirre, Matthews/Boerrigter dk75, Brown, Mulgrew/Biton dk89, Samaras, Commons/Pukki dk77 na Stokes.

Christian Zapata akitimka kushangilia baada ya kuifungia bao la kwanza AC Milan dhidi ya Celtic

Mwafrika hatari: Sulley Muntari wa Milan akishangilia baada ya kufunga bao la pili zikiwa zimebaki dakika tano

Phillipe Mexes akimrukia Cristian Zapata baada ya Mcolombia kufunga

Ukuta mgumu: Wachezaji wa AC Milan wakiwa wameweka ukuta wakati beki wa kati wa Celtic, Charlie Mulgrew akipiga mpira wa adhabu
PANDE ZA DARAJANI
MECHI nne bila ushindi. Kama Rafa Benitez angekuwa bado yupo kazini, anerushiwa mayai viza.
Jose Mourinho amepata kipigo katika mchezo wake wa kwanza wa Ligi ya Mabingwa baada ya Chelsea kuchapwa mabao 2-1 nyumbani na FC Basle.
Oscar alitangulia kuwafungia The Blues dakika ya 45, lakini Salah akasawazisha dakika ya 71, kabla ya Streller kufunga la ushindi dakika ya 82 Uwanja wa Stamford Bridge.
Kikosi cha Chelsea kilikuwa: Cech, Ivanovic, Cahill, Luiz, Cole, Oscar, van Ginkel/Mikel dk75, Lampard/Ba dk76, Willian/Mata dk67, Eto'o na Hazard.
Basle: Sommer, Voser, Schar, Ivanov, Safari, Salah/Xhaka dk88, Diaz, Frei, Stocker/Ajetidk 83, Sio/Delgado dk65 na Streller.

Mkono kichwani: Frank Lampard (kushoto) akionekana mnyonge wakati Basle wanashangilia ushindi wao Stamford Bridge

Wanyonge: Gary Cahill, Oscar na John Obi Mikel wakisikitikia kipigo

Mshii wa mechi: Marco Streller (wa pili kushoto) akiifungia bao la ushindi Basle

Mkali wa vichwa: Streller (katikati kushoto) akishangilia na mfngaji mwenzake Mohamed Salah

Bao: Mohamed Salah (katikati) akishangilia na wachezaji wenzake wa Basle baada ya kusawazisha

La kusawazisha: Mohamed Salah (katikati) alifunga bao zuri

Huzuni tu: Jose Mourinho amefungwa mechi ya pili tangu arejee Stamford Bridge

Ujumbe kwa kocha: Shabiki la Chelsea akipeleka ujumbe kwa kocha Mourinho kwamba Juan Mata anastahili kucheza na si kukaa benchi

Benchi: Nahodha wa klabu, John Terry alisugua benchi

Anapeperusha bendera : Oscar akishangilia baada ya kuifungia Chelsea mwishoni mwa kipindi cha kwanza

Mikogo kwa mashabiki: Kiungo Mbrazil akishangilia bao lake

Oscar anakwenda kufunga

Ashley Cole akipambana na Salah
WATOTO WA WENGER
ARSENAL imeanza vyema Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kushinda ugenini mabao 2-1 dhidi ya wenyeji, Marseille Uwanja wa Velodrome, Ufaransa.
Mabao ya Gunners yalifungwa na Theo Walcott dakika ya 65 na Aaron Ramsey dakika ya 83, wakati la wenyeji lilifungwa na Jordan Ayew kwa penalti dakika ya 90.
Kikosi cha Arsenal kilikuwa: Szczesny, Gibbs, Koscienly, Mertesacker, Sagna, Flamini/Myaichi dk90, Wilshere, Ramsey, Ozil, Walcott/Monreal dk77 na Giroud.
Marseille: Mandanda, Fanni, N'Koulou, Mendes, Morel, Romao, Imbula/Thauvin dk79, Payet/J.Ayew dk72, Valbuena/Khalifa dk89, A. Ayew na Gignac.

Kitu hicho: Theo Walcott ameifungia Arsenal


Kitu kingine: Aaron Ramsey amefunga bao la sita msimu huu


Si mchezo wangu: Mesut Ozil alicheza kiungwana katika ukabaji wake

Kipaji: Theo Walcott akipambana na kiungo wa Marseille, Mathieu Valbuena

Yuko juu: Jack Wilshere alicheza vizuri katika nafasi ya kiungo

Sito rafu? Buti la juu likimuelekea Mathieu Flamini

Rekodi ya klabu: Arsenal imetweet mechi zake 10 ilizoshinda ugenini

Hafunguki kwa urahisi: Steve Mandanda aliibania Arsenal hadi dakika ya 65

Yalaaa: Arsenal walifikiri walistahili kupewa penalti baada ya buti hili alilopigwa Per Mertesacker

Yuko juu: The Gunners ina sababu za kujivunia Ozil

La kufuta machozi: Jordan Ayew akifunga kwa penalti

Mchapakazi: Flamini alionyesha yeye ni mchezaji hodari


Mgumu: Arsene Wenger (kulia) atafurahia Mertesacker na Wojciech Szczesny (kushoto) wasiporuhusu mabao

Nambari moja: Walcott akiupungua umati wa mashabiki baada ya mechi

Alipigana: Olivier Giroud alishindwa, kufunga licha ya kupambana