Like Us On Facebook

MAELFU YA WANANCHI WAJITOKEZA KATIKA MKUTANO WA CHADEMA,NCCR, CUF HUKO JANGWANI JIJINI DAR.


     Maelfu  wakazi wa jiji la Dar es salaam  wengi wao wakiwa ni  wafuasi wa vyama vya Chadema ,Cuf na NCCR Mageuzi  wemefurika katika  viwanja vya jangwani kuwasilikza  viongozi wakuu wa vyama hivyo ambapo kwa pamoja viongozi hao  wanapinga  hatua  ya serikali  kuingiza baadhi ya vipengele  katika mswada wa  sheria  ya marekebisho  ya  sheria  ya mabadiliko ya katiba .

Viongozi  hao  wanadai  kuwa  vipengele hivyo vitapelekea kupatikana kwa katiba  ya upande mmoja  na kuongeza kuwa kama mswada huo hautafanyiwa marekebisho, basi  wao  hawatashiriki katika bunge la katiba.
  
Katika viwanja hivyo  ulinzi uliimarishwa kutoka katika vikundi mbalimbali  vinavyomilikiwa na vyama hivyo  huku shamra shamra za huko na kule zikiwa hazikosekani ili mradi kunogesha mkutano.
 

Mwenyekiti wa taifa wa Chadema  na ambaye  ni kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni Mh Freeman Mbowe amewataka watanzania kuacha uoga na wasimame imara kudai katiba bora.
 

Naye mwenyekiti wa Cuf Mh Profesa Ibrahim Lipumba  amesema Tanzani inahitaji katiba ambayo italinda na kusimamia rasilimali za taifa  kuweza kutimia kwa usawa na kuzingatia mahitaji ya watanzania wenyewe.
 
Kwa upande wake mwenyekiti wa NCCR Mageuzi  na mbuge wa kuteuliwa amesema hakuna haja ya kutumia  mabavu  na badala yake ameitaka serikali itumie busara zaidi ili kuweza kufikia  mwafaka wa jambo hili.

TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari