Like Us On Facebook

BREAKING NEWS:MOTO WAWAKA KARIBU NA JENGO LA BANK YA UBL MKWEPU POSTA


            Moto umeripotiwa alfajiri ya kuamkia Jumapili ya leo katika jingo moja lililopo katikati ya Jiji la Dar es Salaam kwenye mtaa wa Samora na Mkwepu Street.

Kikosi cha Polisi kilifika mapema baada ya kupokea taarifa hizo na kisha kikosi cha zimamoto kilifika kikiwa na huduma moja tu ya gari la maji ya kusaidia kuzima moto huo.

Juhudi hizo ambazo kwa hakika hazikukidhi haja, zililazimu kuomba usaidizi wa kikosi cha zimamoto cha kampuni binafsi ya Knight Support.

Hadi taarifa hii inachapishwa (alfajiri ya saa kumi) juhudi za kuuzima kabisa moto huo zilikuwa bado zikiendelea.

Nimapema sana kufahamu chanzo na hasara iliyosababishwa na moto huo.

Taarifa zaidi zitatolewa na vyombo na mamlaka husika.



TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari