Like Us On Facebook

HOFU YATANDA MENGI YAIBUKA MAUAJI YA MFANYABIASHARA

Moshi. Wafanyabiashara wa madini ya Tanzanite katika miji ya Moshi, Arusha na Mirerani wamedai kutoshtushwa na mauaji ya mfanyabiashara tajiri wa madini katika miji hiyo, Erasto Msuya.
Hata hivyo wamedai kilichowashtusha ni kuuawa kwa kumiminiwa risasi nyingi kwa kutumia bunduki ya kivita aina ya SMG hali inayotoa picha kwamba wauaji walikuwa na hasira iliyopitiliza.

 
“Sisi hatujashtushwa na kuuawa kwake kwa sababu hata kama wangempiga risasi mbili ama tano angekufa lakini kilichotustusha ni kuuawa kwa kupigwa risasi nyingi kiasi hicho,”alidai mmojawao.
Mfanyabiashara huyo ambaye hakutaka jina lake litajwe, alidokeza kuwa marehemu alikuwa amejijengea maadui wengi kutokana na biashara yake ya madini na shughuli nyingine.
Wafanyabiashara wengine waliohojiwa walidai kuna hofu imeanza kujengeka kwamba huenda kukajitokeza mauaji zaidi ya kulipiziana kisasi kati ya wafuasi wa marehemu na waliotekeleza mauaji.
SOURCE:MWANANCHI
TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari